Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, January 2, 2015

HUYU NDIYE MTOTO WA MIAKA 2 ALIYEMUUA MAMA YAKE KWA BASTOLA. SOMA HAPA

Mwanamke mmoja nchini Marekani ameuawa na mwanae wa kiume mwenye umri wa miaka miwili baada ya mtoto huyo kuishika bastola iliyokuwa kwenye mkoba wake na kujifyatua risasi kwa bahati mbaya.
2456558900000578-2891673-image-a-1_1419985471752
Tukio hilo limemhusisha mwanamke mwenye miaka 29, Veronica J. Rutledge mkazi wa Blackfoot, Idaho nchini Marekani.
245645D500000578-2891673-image-a-10_1419985619565
Kwa mujibu wa polisi, mtoto huyo alikuwa amekaa kwenye toroli la super market ya Walmart na kuingiza mkono kwenye pochi ya mama yake ambapo aliishika bastola iliyolipuka. Mwanamke huyo alikuwa akifanya shopping kwenye supermarket hiyo akiwa na wanae wanne.
Tukio hilo limenaswa kwenye video za ukaguzi kwenye supermarket hiyo na baadhi ya wafanyakazi walilishuhudia. Supermarket hiyo ilifungwa baada ya tukio hilo.
Chanzo: Daily Mail

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages