Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, March 25, 2013

RAIS WA CHINA XI JINPING AKABADHI UKUMBI WA KIMATAIFA WA MIKUTANO WA MWL NYERERE KWA RAIS KIKWETE

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ufunguo kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jinping wakati wa makabidhiano ya ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo. Ukumbi huo umejengwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya China na Tanzania.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa China Mhe.Xi Jinping wakiangalia picha za matukio mbalimbali yanayohusu historia ya ushirikiano kati ya China na Tanzania katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere leo wakati wa sherehe za makabidhiano ya ukumbi huo jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa China, Mhe. Xi Jinping pamoja na mkewe katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere muda mfupi baada ya sherehe za ufunguzi wa ukumbi huo leo.
(PICHA NA FREDDY MARO, IKULU)

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages