Beyonce aka mama Blue Ivy alijikuta anashindwa kuficha hasira zake jukwaani baada ya shabiki mmoja huko Denmark kuzidiwa na mzuka wa show yake na kumchapa kofi la kalio mrembo huyo mke wa rapper Jay Z.
Ni jambo la kawaida mwanamuziki anapokuwa ana perform kujaribu kufanya kila aliwezalo kuzidi kuwapagawisha mashabiki ambao hupiga mayowe kama ishara ya kuenjoy kile kinachofanywa na msanii awapo jukwaani. Moja ya vitu wavifanyavyo wasanii wengi huwa ni kushuka jukwaani na kusogea mpaka eneo walipo mashabiki kwa lengo la kuimba nao huku wakimpa mkono.
Kilichomkuta Bey katika concert yake huko Copenhagen, Denmark usiku wa (May 27), wakati aki perform hit song yake ya ‘Irreplaceable’ ni kwamba aliamua kushuka kwa mashabiki ili kuimba nao, ndipo alipojitokeza shabiki mmoja na kumpiga kofi la kalio mke wa Jay Z (pata picha).
Ghafla Bey alisimama na kuacha kuimba, akaitazama mali ya Jigga iliyoguswa kama iko salama! na kisha kumtazama kwa hasira shabiki huyo aliyejichanganya na umati mkubwa wa mashabiki wengine na kumpa maneno machache ya kumtishia kumwondoa shabiki huyo ukumbini hapo “I will have you escorted out right now, alright?”, na akaendelea na show.
Tazama hapa video ya tukio hilo
Post Top Ad
Your Ad Spot
Thursday, May 30, 2013
Home
Unlabelled
VIDEO:BEYONCE ALICHOMWAMBIA SHABIKI HUYU WA KIUME BAADA YA KUMCHAPA KOFI LA KALIO.
VIDEO:BEYONCE ALICHOMWAMBIA SHABIKI HUYU WA KIUME BAADA YA KUMCHAPA KOFI LA KALIO.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.