RAIS
Mstaafu wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela (94) hali yake kiafya
bado tete kwa maradhi ya mapafu na ini yanayomsumbua, hivi sasa amelazwa
katika Hospitali ya Mediclinic Heart jijini Pretoria, Afrika Kusini.
Mzee
Mandela au maarufu kama Madiba historia ya maisha yake ni ndefu, lakini
leo katika safu hii tunapenda kushughulika na picha zinazomuonesha
akiwa katika vipindi mbalimbali katika maisha yake.
Ila kwa ufupi
sana, Mzee Madiba alikuwa mpinzani wa serikali ya kibaguzi nchini mwake,
matokeo yake alifungwa maisha katika Gereza la Kisiwa cha Robben lakini
akatumikia miaka 27.
Akiwa gerezani, kuna taarifa kuwa Mzee Madiba
alitumia blanketi lililotengenezwa nchini Tanzania lenye chapa ya Super
Simba na picha ya mnyama huyo (angalia picha).
Kifungo chake
kilitokana na kupatikana na hatia ya kuhujumu na kula njama ya kuipindua
serikali ya Makaburu. Aliachiwa huru mwaka 1990. Mei 10, 1994
akachaguliwa kuwa rais wa nchi yake akiwa Mwenyekiti wa Chama cha
African Congress Party. Juni 14, 1999 aliacha kugombea nafasi hiyo.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Saturday, June 29, 2013
Home
Unlabelled
NELSON MANDELA: UJANA MPAKA UZEE
NELSON MANDELA: UJANA MPAKA UZEE
Post Top Ad
Your Ad Spot
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.