PICHA: RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA KIKWETE WAKIMFARIJI MJANE NA FAMILIA NZIMA YA BALOZI ISAAC SEPETU


w1

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole mjane wa Balozi Isaac Sepetu, Mama Miriam Sepetu, alipokwenda na Mama Salma nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole kwa mjane huyo na familia ya Marehemu Sepetu aliyefariki jana jijini Dar es salaam.
bofya

w6
w2
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa pole kwa wanafamilia wa Balozi Isaac Sepetu alipokwenda na Mama Salma nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole kufuatia msiba Marehemu Sepetu aliyefariki jana  jijini Dar es salaam.
w3
Mke wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akimfariji mjane wa Balozi Isaac Sepetu alipokwenda  nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole kufuatia msiba Marehemu Sepetu aliyefariki jana katika jijini Dar es salaam
w4
Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa Balozi Isaac Sepetu  alipokwenda  nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole. Marehemu Sepetu aliyefariki jana katika jijini Dar es salaam.
w5
Mama Salma Kikwete  akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa Balozi Isaac Sepetu  nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam. . Marehemu Sepetu aliyefariki jana katika jijini Dar es salaamsource;dewjiblog
Mwili wa marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu utafikishwa nyumbani kwake eneo la Sinza Mori lililoko jijini Dar es Salaam siku ya kesho Jumanne October 29, 2013 kuanzia saa sita za mchana na mwili huo utaanza kuagwa kwenye mida ya saa nane za mchana na baada ya kuagwa mwili huo utafanyiwa maandalizi ya kusafirishwa kwenda Zanzibar siku ya Jumatano asubuhi tarehe 30, October 2013 na mwili wa marehemu ukifika Zanzibar, Unguja utapelekwa  kanisani kwa ajili ya maombi pia utapumzishwa kwenye makazi yake ya daima eneo la Mbozini, Unguja siku ya Jumatano October  30, 2013


Balozi David Kapya akisaini kitabu cha maombolezo ya Marehemu Balozi  Isaac Abraham Sepetu nyumbani kwake eneo la Sinza Mori jijini Dar es salaam leo Jumatatu October 28, 2013


Mke wa marehemu akiwa kwenye majonzi


Wema Sepetu akiwasiliana na ndugu na jamaa kwenye msiba wa baba yake marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu leo October 28, 2013


Mtoto wa maheremu na pia msemaji wa familia Aman Isaac Sepetu akizungumza na vyombo vya habari leo nyumbani kwa marehemu




Balozi David Kapya akibadilishana mawazo na ndugu, jamaa na marafiki kwenye msiba wa marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu leo nyumbani kwake maeneo ya Sinza Mori


Baadhi ya ndugu na jamaa waliofika kwenye msiba


Baadhi ya ndugu na jamaa waliofika kwenye msiba


Baadhi ya ndugu na jamaa waliofika kwenye msiba


Baadhi ya ndugu na jamaa waliofika kwenye msiba




HISTORIA FUPI YA MAREHEMU ISAAC  ABRAHAMU SEPETU

Balozi Isaac Abraham Sepetu alizaliwa October 15, 1943, ni mzaliwa wa Tabora ila alikulia Zanzibar na alikuwa ni mkaazi wa Zanzibar mpaka mauti yanamfika

Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu alipata elimu yake ya msingi na sekondari  katika shule ya St.joseph’s  kwa sasa inaitwa Tumekuja huko Zanzibar mnamo mwaka 1952 hadi 1963, vilevile aliweza kujiunga na chuo kikuu huko Berlin nchini Ujerumani mwaka 1964 hadi 1970 alisomea Shahada ya Uchumi,

Marehemu alikuwa anauwezo wa kuongea lugha tatu (3) kwa ufasaha ambazo ni ;- kiswahili, kingereza  na kijerumani.


KAZI

Alianza kufanya kazi katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar mwaka 1971 hadi 1972 kama Mkuu wa Bizanje Msaidizi na pia alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ikulu. Baada ya hapo mwaka 1972 hadi 1977 alikuwa Naibu Waziri Mambo ya Nje  katika serikali ya Muungano Zanzibar, mnamo mwaka 1977 hadi 1979 Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu  alikuwa Waziri wa Habari na Utangazaji, Ilipofika mwaka 1979 hadi 1982 alikuwa Waziri wa Utalii na Maliasili .

Marehemu Balozi  Sepetu mwaka 1982 hadi 1989 alipewa nafasi ya kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Moscow na mwaka 1989 hadi 1990 alikuwa Balozi wa nchi ya Zaire, Kinshasa


Katika Serikali ya Mapinduzi

Mwaka 1990 hadi 2000 alikuwa Waziri wa Nchi, Mipango pia alikuwa Mshauri wa Rais, Ushirikiano wa Kimataifa na pia alikuwa Katibu , Kamati ya Pamoja(IPC) CCM/CUF, Zanzibar Mwaka 2001 hadi 2005 alikuwa mbunge wa bunge la Afrika ya Mashariki


Uzoefu wa Kisiasa

Mwaka 1977 hadi 2005 alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi


Comments