Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, January 16, 2015

HUU NDIO UKWELI KWAMBA ZARI THE BOSS LADY ANAMIMBA YA DIAMOND!!

Diamond Platnumz na Zari Tlale aka The Bosslady wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza.
10933802_10206026027914724_5426922187710678480_n
Good news hizo zilizotolewa na Diamond mwenyewe kwenye Instagram baada ya kupost picha ya Utrasound aliyotumiwa na mpenzi wake huyo.
zari ultra sound
“I cannot wait to have you on my hand, #Chibu_Junior,” aliandika kwenye picha hiyo.
Hata hivyo Diamond aliifuta picha hiyo kwenye akaunti yake ndani ya dakika mbili tu tangu aipost na hivyo watu wengi wakabakia kusimuliwa tu. Lakini wajanja waliiscreenshot mapema na kukaa na picha hiyo kwenye simu zao.
Kutokana na hali hiyo, baadhi ya watu wameshindwa kuamini taarifa hiyo na wengine wakijiaminisha kuwa ni picha ya dada yake na Diamond, Esma kitu ambacho sio kweli kwakuwa Esma ana mimba kubwa kiasi ambacho picha yake ya Utrasound ingeonesha jinsi mtoto wake alivyo mkubwa. Kingine Diamond hawezi kumuita mtoto wa dada yake ‘Chibu Junior.’
Hebu sasa tuangalie kwa jicho kali zaidi picha hiyo ili tubaini ukweli huu kuwa Diamond atakuwa anaitwa baba takriban miezi minane ijayo.
Tazama juu kabisa ya picha hiyo utaona jina la mhusika wa ultrasound hiyo ni ‘Tlale’ ambalo ni jina laka baba yake na Zari. Umri wake pia umeandikwa kuwa ni miaka 34. Vipimo hivyo vimechukuliwa kwenye hospitali iitwayo Dr Makhubela, iliyopo Soweto nchini Afrika Kusini.
So guys, ile project ya Zari na Diamond imefanikiwa kutengeneza kiumbe kipya. No wonder Diamond amekuwa ni mtu mwenye furaha kubwa kila awapo na mrembo huyo kwakuwa pamoja na kuwa na hamu kubwa ya kuwa na mtoto, warembo aliokuwa nao awali walipendelea kuendelea kula ujana na kumnyima fursa hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages