Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, September 22, 2015

DIAMOND PLATINUMZ: SIJAMLIPISHA MTU PESA KUMUONA LATIFFAH, NI HABARI NA UWONGO.!!

Kwa umaarufu alionao mtoto wa Diamond na Zari, Latiffah Nasib Abdul au kama baba yake anavyopenda kumuita Tiffah, ni wazi kwamba mashabiki wengi wa staa huyo wangependa kumuona ama kumbeba mtoto huyo aliyejipatia umaarufu toka siku yake ya kwanza duniani.
diamond na Tiffah
Hiyo inatokana pia na uamuzi wa wazazi wake kutomuonesha mapema sura yake hadi Jumapili iliyopita, ambayo iliongeza shauku hiyo.
Licha ya kuwa picha za kwanza kuonesha sura zake zilidhaminiwa na makampuni, lakini Dimond amekanusha uvumi kuwa anatoza kiasi fulani cha fedha kwa watu wa kawaida ambao wangepeda kumuona Tiffah uso kwa uso. Diamond Ameiambia BBC kuwa habari hizo ni za uongo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages