Mhe. Chande akipokelewa na Bw. Suleiman Saleh,Afisa Ubalozi wa Tanzania Washington DC
Mhe. Chande akisaini kitabu caha wageni Ubalozini hapo.
Mhe.Chande akiwa na Bw.Suleiman Saleh mara baada ya kumaliza ziara yake Ubalozini
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe.Mohamed Othman Chande yuko ziarani nchini
Marekani ziara ambayo imejumuisha Majaji Wakuu wengine kutoka Afrika
Kusini,Ghana,Namibia,Zanmbia,Malawi,Kenya,Uganda
na Msumbiji, Ziara hii ya aina yake imeratibiwa na Wizara ya Mambo ya
Nje ya Marekani na madhumuni yake makubwa ni kujionea jinsi mfumo wa
Sheria na Utoaji Haki katika mahakama vinafanya kazi pamoja na maeneo ya
Utawala Bora. Katika ziara hii Jaji Mkuu Chande ametembelea mahakama ya
Rufaa ya Marekani jijini Washington DC pamoja na Chuo Endelevu cha
Majaji Chicago na leo hii alionana na Mhe.Hilary Clinton, Waziri wa
Mambo ya Nje wa Marekani pamoja na Majaji wengine waalikwa na kuwa na
mazungumzo nae katika Wizara ya Nje ya Marekani Washington DC.
Mhe.Mohamed Othman Chande PIA alipata wasaa wa kutembelea Ubalozi wa Tanzania Washington DC..
No comments:
Post a Comment