Msemaji katika Hafla ya Women in
Balance Kitchen Party Gala Mhadhiri Msaidizi wa Idara ya Saikolojia
katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Bw. Chris Mauki akitoa somo la
Saikolojia kwa wakinamama na wasichana waliohudhuria hafla hilo
iliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee VIP Hall jijini Dar.
Life Style Designer of Sex and
Relationships kutoka Kenya Bi. Getrude Mungai akitoa somo la kuhusiana
na masuala ya mahusiano ya kimapenzi kwa wenye ndoa na wasiokuwa na ndoa
ambapo amesema vipo vitu vingi vinavyochangia kuboresha ama kuharibu
mahusiano hayo ambapo wahusika wanatakiwa kuvifahamu na kuvitilia mkazo
ili kudumisha mahusiano yao.
Mafunzo kwa vitendo yalihusika pia.
Msemaji wa mwisho alikuwa ni
Mama Veronica aliyewaacha hoi kwa vicheko wanawake waliohudhuria Kitchen
Party Gala ambapo alizungumzia masuala ya uvumilivu katika ndoa sio tu
kukosekana kwa kipato ndani ya nyumba bali hata mikimiki ya Unyumba kwa
wanandoa.
Independent Sales Consultant wa
bidhaa za Oriflame Bi. Jesca Mwakyulu akionyesha bidhaa ya Feminele
Intimate Wash ya Oriflame ambayo ameisifia kuwa na Natural Lactic Acid
ambayo inasaidia kutunza hali halisi ya sehemu za siri za Mwanamke.
Amefafanua kuwa kwa asili sehemu
hizo zina hiyo Lactic Acid ambayo hutunza unyevu sahihi na Bacteria
wazuri ambao husaidi kutoa ulinzi dhidi ya Fangasi, miwasho na harufu
mbaya.
Mmoja wa wadhamini wa Women in
Balance Kitchen Part Gala Mwakilishi kutoka TSN Super Market Lizbeth
akitangaza zawadi kumi kwa wageni waliohudhuria Kitchen Party Gala
zikiwemo Vocha za kufanya Shopping katika Super Market za TSN zilizopo
jijini Dar es Salaam.
Wakinadada wakionekana kufurahishwa na mambo yaliyokuwa yakizungumziwa kwenye Kitchen Party Gala hiyo.
Mkurugenzi wa Prime Time Promotions, Juhyna Kusaga (kushoto) na mdogo wake.
Kwa picha zaidi bofya read more
No comments:
Post a Comment