* Wajumbe ukumbini wamwita 'jembe'NA MWANDISHI WETU
* Anogesha mkutano kwa kucharaza gita na Vijana Jazz
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye,
amenogesha Mkutano mkuu wa nane wa Umoja wa Vijana wa CCM, UVCCM
unaoendea mjini Dodoma.
Licha ya viongozi wengi kushangiliwa wakati wa kuingia ukumbini,
nderemo na shamaramshamra zililipuka zaidi kutoka kwa wajumbe wa
Mkutano huo wakati Nape alipotangazwa kuwasili.
"Jembe, jembe, jembe", wajumbe walisikika wakilipuka na kumshangilia
baada ya Mkuu wa Umahasishaji na Chipukizi wa UVCCM, Esther Bulaya
alipotangaza kuwasili kwa Nape ukumbini.
No comments:
Post a Comment