Ndege ndogo ya kijeshi ya mazoezi, (Military training aircraft) namba
JW 9129, iliyokuwa ikitumiwa na marubani wanafunzi wa jeshi hilo, baada
ya kupoteza muelekeo na kugonga kontena kwenye eneo la uwanja wa ndege
wa Julius Nyerere eneo la Airwing Ukonga Jijini Dar es Salaam jana.
Mwanajeshi mmoja Kepten Deogratius Magushi, alipoteza maisha wakati yeye
na mwenzake Kepteni Feruzi Kwidika, walipojaribu kujiokoa kwa kutumia
miavuli ya usalama ambapo Kepteni Magushi alirushwa na kudondoka juu ya
paa la jengo moja ndani ya uwanja na kupoteza maisha, Msemaji wa JWTZ,
Kanali Kapambala Mgawe alithibitisha jana. (Picha kwa hisani ya JWTZ)
Ndege ya kivita ya Jeshi la Ulinzi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ) imeanguka na kusababisha kifo cha mwanajeshi
mmoja na kujeruhiwa mmoja wakati wakiwa katika mafunzo ya kurusha
ndege.
Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe, akizungumza na NIPASHE alithibitisha kutokea kwa tukio hilo jana majira ya saa 4:28 asubuhi makao makuu ya kambi ya Jeshi la Anga (Air Wing) eneo la Ukonga, jijini Dar es Salaam.
Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe, akizungumza na NIPASHE alithibitisha kutokea kwa tukio hilo jana majira ya saa 4:28 asubuhi makao makuu ya kambi ya Jeshi la Anga (Air Wing) eneo la Ukonga, jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment