Waziri wa uchukuzi Haryson Mwakyembeakipanda treni ya tazara wakati wa
uzinduzi maalum ya usafiri dar es salaam kutoka katika stesheni ya
tazara kuelekea mwakanga katika ahadi ya serikali ya usafiri treni
katika pembezoni mwa jiji LA DAR ES SALAAM LEO
BAADHI YA ABIRIA WAKIPANDA TRENI YA USAFIRI MAALUM WA TRENI KATIKA JIJI
LA DAR ES SALAAM KUTOKA TAZARA KWENDA MWAKANGA NJE KIDOGO YA JIJI LA
DARES SALAAM WAKATI WA UZINDUZI LEO
BAADHI YA WAKAZI WA YOMBO RELINI KIWALANI WAKI FURAHIWA USAFI RI WA
TRENI MPYA YA DALADALA YA TRENI KUTOKA TAZRA MPAKA MWAKANGA LEO
Wanacheeeeeeeeka...! Abiria wakifurahia usafiri wa treni. (Picha: Kwa hisani ya issamichuzi.blogspot.com)
Ndani ya daladala la treni ni hakuna vurugu wala longolongo... ni raha eeenh! Hivi ndivyo ilivyo ndani ya chombo.
Chombo kikikatiza mitaa.
Mchuma wa Tazara utakaotumika kama daladala kutoka eneo la Tazara hadi Mwakanga.
Hatimaye ile ahadi ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe
kuhusiana na kuanzishwa kwa usafiri wa daladala za treni jijini Dar es
Salaam imeanza kutekelezwa leo asubuhi na wananchi mbalimbali
wakanufaika na huduma hiyo kwa usafiri kati ya Ubungo Maziwa na
Stesheni.
Usafiri mwingine wa treni uliozinduliwa leo jijini Dar es Salaam ni wa kupitia reli ya Tazara, kutoka Tazara hadi Mwakanga.
Akizungumza wakati wa kuzindua rasmi safari hizo leo, Dk. Waziri
Mwakyembe aliwataka wananchi watakaokuwa wakitumia usafiri huo kuvumilia
kasoro mbalimbali zitakazojitokeza katika siku za mwanzo na kuahidi
kwamba serikali itaendelea kuboresha huduma hizo kila uchao.
Dk. Mwakyembe aliwataka wakazi wa Dar es Salaam, hasa kwenye maeneo
yaliyo karibu na reli kutunza miundombinu ya usafiri huo, ikiwa ni
pamoja na kukomesha tabia ya baadhi ya watu kugeuza maeneo ya njia za
reli kuwa majalala ya kutupia uchafu.
Akawataka viongozi wa serikali za mitaa ambako reli zinapita waongoze
uangalifu ili usafiri huo uendelee vyema na kuwapunguzia adha ya usafiri
na foleni wakazi.
"Inasikitisha kuona kuwa katika baadhi ya maeneo, reli zimegeuzwa kuwa
dampo na kujaa uchafu... nawaomba tujitahidi kutunza maeneo haya ya
miundombinu ya reli," akasema Dk. Mwakyembe.
Katika hatua nyingine, Waziri Mwakyembe aliwapongeza mafundi wa TRL na
Tazara kwa kufufua mabehewa 14 yaliyokuwa yamekufa kabisa na kuokoa Sh.
bilioni 2.1
Alisema vilevile kuwa vichwa vya treni vilivyofufuliwa na mafundi wa
mashirika hayo na miundombinu mingine imeokoa jumla ya Sh. bilioni 18.
"Hivi vichwa peke yake, kama vingekodishwa vingetugharimu kati ya Sh. bilioni 9 au 10 hivi," alisema Dk. Mwakyembe.
No comments:
Post a Comment