Mawakili wa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Abdallah Juma kushoto na Salim
Tawfik wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu nia yao ya kujitoa
kwao siku ya leo katika kesi hiyo kutokana na kile walichoita usumbufu
wanaofanyiwa wateja wao wa kuhangaishwa na kukosa kupelekwa Mahakama ya
Kwerekwe kwa muda muafaka
Kiongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Sheikh Farid Hadi Ahmed kushoto akiwa na
wenzake sita walioletwa Mahakama kuu Zanzibar Vuga wakiwa hawana ndevu
na kufunguliwa mashtaka manne mapya mahakamani hapo yakiwemo kuharibu
mali za watu zenye thamani ya Shl.Milioni 50 na kufanya vurugu za
makusudi zakuhatarisha amani katika nchi
Baadhi ya Askari wa kutuliza fujo wakiwa Mahakama kuu Zanzibar Vuga kwa lengo la kulinda usalama na amani Mahakamani hapo
Baadhi ya Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO wakiwa wanatoka katika Mahakama
Kuu ya Zanzibar Vuga baada ya kufunguliwa mashtaka manne mapya..Picha na
Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar
Na Salma Said
VIONGOZI wanane wa Jumuiya za Uamsho
na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) huku wakiwa wamenyolewa ndevu
wameshitakiwa mahakamani kwa madai ya kuhatarisha amani Zanzibar.
Wakitarajiwa kufikishwa
mahakamani jana kuendelea na kesi yao ya awali kwenye Mahakama ya Wilaya
ya Mwanakwereke, viongozi hao walipelekwa Mahakama Kuu Vuga mjini hapa
na kufunguliwa mashitaka mapya.
No comments:
Post a Comment