Ni muda umepita hatujasikia story kuhusu wawakilishi wa Tanzania katika Big Brother toka Feza aponee katika tundu la sindano kuiaga $300,000. Lakini kipenzi cha kinadada kijana mtanashati na ‘handsome’ Nando ameibuka na lake baada ya kuanza kuonesha hitaji la kuondoka South Afrika akiwa na kumbukumbu ya mchoro katika mwili wake (Tattoo).
Wakati wenzake mjengoni wanakimbizana na mapenzi yeye mapenzi yake hivi sasa ni juu ya mwili wake kupata mchoro ‘Tatoo’. Akiwa katika Diary Session Nando alimwomba Big Brother amletee mtu wa kumchora Tattoo mjengoni. Baada ya ukimya bila kumwona mchora Tattoo akija mjengoni, Nando akiwa katika diary session nyingine alimkumbushia tena Big Brother juu ya ombi lake la kuletewa mtu wa kumchora Tattoo.
Well, inavyoonekana ugonjwa wa Tattoo baada ya kukosa tiba ya haraka kwa mgonjwa wa kwanza (Nando) hatimaye virusi vikaanza kuenea katika nyumba ya diamond na kumpata mshiriki mwingine wa Botswana Motamma ambaye alimuunga mkono Nando baada ya kumwomba na yeye Big Brother amfanyie favor ya kumletea mtu wa kumchora Tattoo mjengoni hapo.
Siku Nando akirejea Tanzania iwe na kitita cha $300,000 au laa ukiona mwili wake una Tattoo basi ujue kampeni yake na Motamma ya kuomba kuletewa mchora Tattoo mjengoni ilifanikiwa.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Sunday, June 16, 2013
Home
Unlabelled
BIG BROTHER:NANDO WA TANZANIA AMUOMBA BIG BROTHER AMLETEE MCHORA TATOO MJENGONI
BIG BROTHER:NANDO WA TANZANIA AMUOMBA BIG BROTHER AMLETEE MCHORA TATOO MJENGONI
Post Top Ad
Your Ad Spot
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.