Tajiri namba 107 nchini Marekani (kwa mujibu wa Forbes), Paul Tudor Jones II, mwanzilishi wa kampuni ya Tudor Investment Corporation ndiye mwenyeji wa Malkia wa Talk Shows duniani, Oprah Winfrey aliyekuja Tanzania na kufikia mbugani, Serengeti.
Paul Tudor Jones
Oprah aliyetua Serengeti weekend hii alikuwa anatokea nchini Hispania na amekuja Tanzania kwa ziara binafsi. Alipokelewa na naibu waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
Oprah Winfrey
Jones ambaye ana utajiri ufikao dola bilioni 3.3 ambao unamfanya pia awe tajiri wa 330 duniani, ni mwekezaji mkubwa huko Serengeti. Tajiri huyo ndiye mmiliki wa hoteli za kifahari mbugani huko za Singita Grumeti Reserves (SGR) ambazo zinajumuisha hoteli za , Sasakwa, Farufaru, Sabora Tented Camp na Singita Explore Mobile Camp.
Serengeti Grumeti Reserves
Kwa mujibu wa jarida la Travel- Leisure la Marekani, hoteli hizo zinakamata nafasi ya kwanza kwa miaka miwili mfululizo kati ya hoteli 100 bora duniani.
Tudor Jones anamiliki acre 340,000 kwenye mbuga hiyo ya wanyama ya Serengeti. Tajiri huyo ndiye aliyedhamini ujenzi wa uwanja wa ndege uliopo Mugumu, Serengeti.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Monday, July 15, 2013
Home
Unlabelled
TAJIRI WA 107 MAREKANI "PAUL TUDOR JONES II'' NDIO MWENYEJI WA OPRAH WINFREY ALIYETUA SERENGETI-TANZANIA
TAJIRI WA 107 MAREKANI "PAUL TUDOR JONES II'' NDIO MWENYEJI WA OPRAH WINFREY ALIYETUA SERENGETI-TANZANIA
Post Top Ad
Your Ad Spot
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.