Joh Makini na Ommy Dimpoz wakiwa wamevaa miwani za Weusi
Akiongea na Bongo5, Joh Makini amesema miwani hizi zitaingia rasmi sokoni wiki hii. “Ile alidesign mshkaji wetu mmoja wa Arusha, alicreate hiyo akachukua miwani fulani plain akatengenezea maandishi fulani ambayo yanasomeka ‘Gere’ kwenye hizi glass,” amesema Joh.
“Alivyoileta tukaona ni poa tukaingiza kwenye bidhaa za Weusi,”ameongeza. Joh Makini amesema wiki hii watatangaza bei ya miwani hizo za rangi nyeusi. Hadi sasa bidhaa za brand ya Weusi ni kofia, tracksuit, top na t-shirt.
“Zinaenda poa sana kwa mfano mzigo tulioenda nao Moshi juzi kwenye tour za Kili ziliishia pale pale uwanjani kwahiyo utaoni ni jinsi gani watu bado wana kiu za kuvaa brand ya Weusi.”
No comments:
Post a Comment