Mbunge
wa Arusha Mjini (Chadema) Godbless Lema (wa tatu kushoto) akiwa pamoja
na Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika (wa pili kushoto)
wakielekea makao makuu ya chama hicho baada ya ushindi wa rufaa ya Lema
leo jijini Dar.
---
MAHAKAMA
ya Rufaa Tanzania, leo imetoa hukumu ya rufaa ya kesi iliyokuwa
inamkabili aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema,
Godbless Lema, ambapo imemrudishia kiti hicho cha Ubunge. Mahakama
imejiridhisha kuwa madai ya udhalilishaji hayakuathiri uchaguzi wala
mlalamikaji. Walalamikaji wameamriwa kulipa gharama za kesi hiyo tangu
ilipofunguliwa mpaka ilipoishia.
No comments:
Post a Comment