Walipokaribia katika Serikali ya Mtaa huko Ekwusigo, Sunday Eze alimgeuka mkewe na kuanza kushambulia alimpiga na chuma na kisha kummwagia tindikali mwilini.
kama vile haitoshi baada ya kipigo hicho Sunday Eze alichukua kiasi cha tindikali kilichokuwa kimebakia na kisha kumnywesha mkwe kwa lazima, Ndipo mwanamke huyo alipopiga mayowe ambapo polisi waliokuwa wanapita karibu na eneo hilo walifika mara moja na kukuta mwanamke huyo akiria kwa uchungu huku mumewe akiwa kasha kimbia muda mrefu.
Polisi walimchukua mwanamke huyo na kumkimbiza katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Nnewi iitwayo "Nnamdi Azikiwe" lakini kwa bahati mbaya mwanamke huyo alipofikishwa hospitalini hapo alifariki dunia.
Kwa mujibu wa baba mkwe anadai baada ya kufanya unyama huo Sunday aliwaita wanafamilia siku ya tar 13 october kwa lengo la kutaka kukutana nao na kuwaomba msamaha kwa kitendo alicho fanya lakini hakutaka kusema ni kwa nini alimfanyia unyama huo mkewe.
No comments:
Post a Comment