Mwandishi wa habari, Ephraim Kibonde jana aliachiwa kutoka Kituo
cha Polisi Oysterbay, Dar es Salaam alikokuwa akishikiliwa tangu
mwishoni mwa wiki kwa tuhuma za kusababisha ajali ya gari na kutoa lugha
ya matusi kwa askari wa usalama barabarani
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Camillius
Wambura alithibitisha jana kukamatwa kwa Kibonde na kwamba walikuwa
wakiendelea kufanya uchunguzi wa tukio hilo.
Hata hivyo taarifa zilizopatikana jana jioni zilidai kuwa Kidonde aliachiwa kwa dhamana wakati uchunguzi ukiendelea.
No comments:
Post a Comment