Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, October 11, 2014

MZEE MAJUTO AJIPANGA KUFANYA MOVIE PAMOJA DIAMOND NA WEMA

Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho nchini, King Majuto amesema hivi kariburi alimshawishi Wema Sepetu azungumze na mpenzi wake Diamond Platnumz ili wafanye kazi ya pamoja.
10508029_840308722676521_383474538_n
Diamond na Mzee Mjuto

Mzee Majuto ambaye ni mshindi wa Tuzo za Watu 2014 ya filamu inayopenda, ameiambia Bongo5 kuwa amemwachia kazi hiyo Wema ili azungumzee na mzee (Diamond).
“Hivi karibuni nilikuwa na Wema, nimemwambia aongee na Diamond ili tufanye filamu ya pamoja,” amesema Majuto. “Mimi, Wema na Diamond, hata Diamond ninaweza kuzungumza naye sema nimeanza na Wema kwanza, akikubali mtasikia tu.”
Kwa upande mwingine Majuto amesema ili acheze filamu anahitaji kulipwa shilingi milioni 3.
“Umri unaenda sasa biashara za nisaidie nisaide hakuna, kama unanitaka ili tufanye kazi unatakiwa uandae milioni 3.”

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages