Kwa mujibu wa mmoja wa mameneja wa Diamond Platnumz, tweet zenye hasira zilizoandikwa na Davido jana hazimhusu muimbaji huyo wa ‘My Number One.’
Mitandao mikubwa ya Nigeria ikiwemo Pulse na News24
imeandika kuwa tweets hizo ambazo Davido anamzungumzia mtu asiye na
shukrani kwake na kwamba kiama chake kinakuja, zimemlenga Diamond.
Ur downfall is coming u bastard ungrateful broke fool!!
— Davido (@iam_Davido) January 6, 2015
Meneja wa Diamond, Salam aka ML Eight ameiambia Bongo5 kuwa hakuna ugomvi wowote uliopo kati ya mastaa hao na kwamba wako poa.
Niggas forget who helped them ….. So quick …. God don bless me I do my thing dey go keep my name out ur mouth !! WHO U DON HELP IDIOT!
— Davido (@iam_Davido) January 6, 2015
Uhusiano kati ya mastaa hao wawili uliingia dosari siku ya fainali ya shindano la Big Brother Africa ambapo baada ya Idris kushinda Davido alitweet ‘And They Cheat Again’ na Diamond ambaye usiku huo alishinda tuzo ya TFA za Nigeria aliijibu kwa ujumbe wa kuibeza.
Kufuatia tweet hiyo ya Davido, watanzania wengi walimshambulia kwa matusi na kumtaka aombe radhi kitu ambacho aligoma kufanya.
Tangu hapo, kumekupowepo na speculations kuwa uhusiano kati ya wawili hao umevunjika na ndio maana imekuwa rahisi kwa wengi kuhusi tweet hizo za jana zimemlenga Diamond.
No comments:
Post a Comment