Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, June 1, 2015

WALE WAPENZI WA "EMPIRE SEANON 2" ITAANZA TAREHE HII HAPA. SOMA HAPA.

Kama wewe ni shabiki wa series ya Kimarekani iliyojizolea umaarufu mkubwa mwaka huu ya Empire, habari hii ni njema kwako. Tarehe ya kuanza kwa msimu wa pili wa series hiyo tayari imewekwa wazi.
Empire-Season-2
Co-Starring wa Empire, Taraji P.Henson maarufu kwa jina la Cookie analotumia kwenye series hiyo, ameshare na followers wa Twitter tarehe ya kuanza kwa msimu wa pili ambayo ni September 23, 2015.
Miongoni mwa mastaa waliotangazwa kuwa wataonekana katika msimu wa pili ni pamoja na mchekeshaji Chris Rock, muimbaji Alicia Keys na Lenny Kravitz, kwa mujibu wa mtandao wa AccessHollywood.
empire1
Kutoka kushoto ni Hakeem, Jamal, Cookie na Lucious
Msimu mpya wa show hiyo unatarajiwa kuwa na episode 18 kutoka 12 zilizokuwepo msimu uliopita.
Series hiyo imekuwa gumzo kwa muda mfupi tu toka ilipozinduliwa January 7, 2015, si tu Marekani bali hata sehemu nyingi za dunia.
Empire imechezwa na Lucious (Terrence Howard) anayeigiza kama mmiliki wa label ya muziki inayoitwa Empire, akiwa na watoto wake watatu Adre (Trai Byeres), Jamal (Jussie Smollett) ambaye ni shoga lakini anauwezo mkubwa sana wa kuimba, na wa mwisho anaitwa Hakeem (Bryshere Gray) ambaye ni rapper. Yupo pia mke wa Lucious, Cookie ambaye ameonekana kuwa kivutio cha wengi katika msimu uliopita.
Ingia hapa kuifahamu zaidi Empire.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages