Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, July 5, 2015

HAWA NDIO WABUNGE 35 WA UKAWA WALIOFUKUZWA BUNGENI.


Wabunge  35 wa kambi ya upinzani bungeni jana walitolewa nje ya ukumbi wa bunge na spika wa bunge  Anne Makinda na kupewa adhabu ya  kutokuhudhuria vikao vitano kwa madai ya kukiuka kanuni za bunge .

Mara baada ya kikao cha bunge kuanza spika wa bunge alinza kwa kuwakumbusha wabunge namna ya kufuata kanuni hasa pale wanapotaka kuondoa muswada wowote.

Hali ilibadilika ghafla Bungeni baada ya Mbunge Ezekiel Wenje kuomba Spika atoe ufafanuzi wa kwanini Mbunge Silinde hayuko kwenye list ya waliotajwa kusimamishwa lakini Askari wa Bunge wamemzuia asiingie kwenye Kikao?

Majibu ya Spika hayakuwaridhisha baadhi ya Wabunge, zikaanza tena kelele… ndipo spika aliamua  kuwatoa nje.

Hata hivyo baada ya vurugu zote kuisha miswada yote mitatu ambayo ni  ya sheria ya petroli, sheria ya usimamizi wa mapato ya mafuta na gesi pamoja na sheria ya uwazi na uwajibikaji katika tasnia ya uchimbaji Tanzania iliwasilishwa Bungeni.

Majina ya Wabunge waliotimuliwa  ni,
Ezekiel Wenje
Mussa Kombo
Masoud Abdallah Salim
Rebecca Ngodo
Sabrina Sungura
Khatib Said Haji
Dr. Anthony Mbassa
Maulidah Anna Valerian Komu
Kulikoyela Kahigi
Cecilia Pareso
Joyce Mukya
Mariam Msabaha
Grace Kiwelu
Israel Natse
 Mustapha Akonaay
Konchesta Rwamlaza
Suleiman Bungura
Rashid Ali Abdallah
Ali Hamad
Riziki Juma
Rukia Kassim Ahmed
Azza Hamad
Khatibu Said Haji
Kombo Khamis Kombo
Ali Khamis Seif
Haroub Mohammed Shamisi
Kuruthum Jumanne
Mchuchuli
Amina Mwidau
Mkiwa Kimwanga
Salum Baruhani
Marry Stellah Malaki
Rashid Ally Omary
Mwanamrisho Abama
Lucy Owenya

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages