Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, July 13, 2013

TAIFA STARS LAYAZWA 1- 0 DHIDI YA UGANDA.



Mtanange wa Stars na The Cranes ukiendelea.
Stars wakiwa vichwa chini baada ya matokeo ya leo.
MATUMAINI ya timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kushiriki fainali za CHAN nchini Afrika Kusini imefifia baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes'. Taifa Stars imelala katika mechi ya kwanza iliyopigwa leo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kwa matokeo hayo, Stars inasubiri mechi ya pili itakayopigwa jijini Kampala wiki mbili zijazo na kama itafanikiwa kuibuka kifua mbele zaidi ya matokeo ya leo itakuwa na uhakika wa kushiriki fainali hizo ila kama matokeo yatakuwa vinginevyo basi safari ya Stars itakuwa imeishia hapo.

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages